Hadithi zinaweza kubadilisha maisha yako


Hakuna mtu hapa duniani anayeponyoka kutoka kwa matukio ambayo yalimsababisha maumivu na unyanyasaji kutoka kwa watu tofauti ambao ni mbali au hata karibu sana na sisi. Kwa ujumla, matukio haya huacha ndani yetu makovu na vidonda moyoni mwetu ambavyo vinabaki hata na wakati unaopita. Ni ngumu zaidi wakati chuki kwa watu hawa inatuongoza kulipiza kisasi. Kisasi hiki ni hatari kwa ubinafsi wetu kwa sababu hisia hizi za kulipiza kisasi zinaweza kuathiri matendo na maamuzi yetu kwa kila mtu karibu nasi. Kwa kuongezea, kulipiza kisasi hiki kunasababisha turuba ya giza ambayo huua hisia zote za wanadamu na inaweza kuharibu uwetu wetu kama vile wakati wetu ujao na maisha yetu yote. Nguvu ya msamaha inatupa uhuru kutoka kwa chuki. Watu ambao wamepigana wakawa huru na amani katika mioyo yao na roho. Ushuhuda huu unathibitisha nguvu ya uponyaji ya Mungu, iliyo ndani ya watu kugusa kwa upendo na huruma; hii pia iliiponya mioyo yao, ilibadilisha maisha yao na ikawasamehe. Haijalishi uzoefu wako, asili yako, ngono, unaangaziwa na ugunduzi mkubwa zaidi duniani upendo wa Mungu na fanya mazoezi ya msamaha katika maisha yako mwenyewe.

Hadithi

MESHAK SALUM HASANI
 
MESHAK SALUM HASANI
“Nilionekana kuipenda dini yangu toka utotoni. Na, hata, nilipopelekwa madrasa, nilijisomea kwa bidii na kufikia darasa la sita la Kiarabu.Toka wakati huo, niliendelea na kufuzu kama ustadhi. Kwangu, mimi, dini ilikuwa kila kitu.” Mungu katika ndoto na alinimbia, ‘Hassan, usipoacha uchawi utakufa!’ Sauti ile ilinikosesha amani. Nililazimika kwenda kwenye maombi mlimani, kwa miezi miwili mfululizo,nikimlilia Mungu. Baada ya muda,Mungu alinitahadharisha, ‘Ukitafuta kanisa, litakusaidia.’
USHUHUDA WA MUNA LOVE
 
USHUHUDA WA MUNA LOVE
“MUNGU anazo njia nyingi anazotumia kuokoa watu wake, kwa ajili ya kusudi lake mwenyewe. Alimtumia mtoto wangu akiwa na umri wa miaka sita, kugeuza mtazamo wangu wa imani, siku chache baadaye Mungu alimtwaa. Machungu ya kumpoteza yanazimwa na kauli zake zilizoungamanishwa na upendo wa Mungu ulionivuta mimi kwenye wokovu. Natatangaza fadhili za Bwana katika maisha yangu yote!
ASKOFU JOHN SAID MAGENYEKA
 
ASKOFU JOHN SAID MAGENYEKA
Nilipokuwa katika njiapanda ya udini, huku moyoni nikitaabika kuhusu imani ya kweli, nilimuomna Mungu, anionyeshe njia sahihi itakayoniweka huru mbali na jehanamu ya moto inayokuja. Nikiwa katika dimbwi la mawazo Mungu kupitia ndoto akanionesha njia ya kweli, ninayoisimulia leo.
COSMAS CHIDUMULE
 
COSMAS CHIDUMULE
Maisha ya starehe nyingi, nilipokuwa katika ulimwengu wa muziki duniani hayakunifanya nifikie kwenye utoshelevu wa furaha na amani ya kweli moyoni mwangu. Nilipokutana na Yesu na kubadilishwa mwelekeo nikagundua kuwa, furaha na amani ya kweli inapatikana kwake. Sasa naishi nikiwa na matumaini makubwa ya maisha ya milele.
JAMES YUSTA
 
JAMES YUSTA
Mimi, tofauti na watoto wengine, sikubahatika kumpata mzazi ambaye angenieleza kwa usahihi kuwa nilizaliwa lini na tarehe ngapi! Hata hivyo, ninamshukuru Mungu kuwa nilifanikiwa kupata sehemu ndogo tu ya historia ya maisha yangu, kama nilivyosimuliwa na mama mmoja aliyejulikana kwa jina la YUSTA, aliyeniokoa kutoka katika kinywa cha mbwa aliyekuwa katika hatua za mwisho akitaka kunitafunatafuna!
DK. JOE MZIWANDA (Kiongozi wa Dini)
 
DK. JOE MZIWANDA (Kiongozi wa Dini)
Mafanikio bila Mungu sawa na kujilisha upepo. Ni kuwa na furaha bila amani ya kweli. Niliishi maisha ambayo, licha ya kuwa yenye furaha, sikupata amani ya moyo. Hii ilinipelekea kuwaza sana siku moja na, hatimaye, niliamua kuchukua maamuzi sahihi. Maamuzi yale ndiyo yaliyoniwezesha kupata amani iliyoambatana na furaha niliyoitafuta kwa muda mrefu.”
USHUHUDA WA BAHATI JOSEPH ONGONG’A
 
USHUHUDA WA BAHATI JOSEPH ONGONG’A
Amani, furaha na tumaini ziliyeyuka katika maisha yangu, hayo ni baada ya ajali mbaya ya gari iliyopelekea kukatwa mguu wangu wa kulia na kuniachia mateso na maonzi mengi. Lakini ashukuriwe Mungu wangu, aliyeniinua tena kutoka mavumbini, na kunirejeshea tumaini jipya lenye furaha na amani tele yanayonifanya nisonge mbele hata katika hali hii niliyo nayo. Nikutie moyo wewe unayepitia mateso pengine kama niliyopitia au zaidi, kuacha kulalamika na kuona tatizo lako kama mlina mkubwa na ugeuze macho yako sasa ukamatazame Mungu, aliye msaada wetu
MASULU MAKASSY
 
MASULU MAKASSY
“… Kupitia muziki, nilijipatia marafiki wengi sana, akiwemo Idd Amin Dadaa, kabla ya kumpindua Milton Obote na kuutwaa Urais wa Uganda. Pamoja na hayo nilipitia mambo magumu na mazito katika maisha yangu nikiwa nchini, Uganda, ikiwamo kuwekwa maabusu chumba kidogo pamoja na maiti kwa siku tatu! Baada ya kumpokea Kristo, Bwana na Mwokozi wa maisha yangu, niliamua kumtumikia Mungu kwa njia ya uimbaji.”
BOAZ DAVID MWASOTA
 
BOAZ DAVID MWASOTA
Maisha ya kutumia mihadarati na uporaji yalinitenga mbali na familia. Jamii yangu ilinichukulia kuwa kama ‘mbwa mwitu,’ aliyeishi katikati ya watu. Niliadahika nikidhani kuwa, kwa kufanya hivyo, ningeondokana na upweke. Kumbe haikuwa hivyo! Nilijiongezea matatizo yaliyochangia kujiangamiza kimaisha. Ashukuriwe Mungu aliyeniona, tokea mbali na kunivuta ili kuniingiza katika pendo lake na kuniondolea aibu, leo nathubutu kusimulia matendo yake makuu.”

Agiza zawadi yako

    Ingiza jina lako kamili

    Ingiza barua pepe halali

    Kwa MkonoToa kwa Chapisho