Hadithi zinaweza kubadilisha maisha yako

Hakuna mtu hapa duniani anayeponyoka kutoka kwa matukio ambayo yalimsababisha maumivu na unyanyasaji kutoka kwa watu tofauti ambao ni mbali au hata karibu sana na sisi. Kwa ujumla, matukio haya huacha ndani yetu makovu na vidonda moyoni mwetu ambavyo vinabaki hata na wakati unaopita. Ni ngumu zaidi wakati chuki kwa watu hawa inatuongoza kulipiza kisasi. Kisasi hiki ni hatari kwa ubinafsi wetu kwa sababu hisia hizi za kulipiza kisasi zinaweza kuathiri matendo na maamuzi yetu kwa kila mtu karibu nasi. Kwa kuongezea, kulipiza kisasi hiki kunasababisha turuba ya giza ambayo huua hisia zote za wanadamu na inaweza kuharibu uwetu wetu kama vile wakati wetu ujao na maisha yetu yote. Nguvu ya msamaha inatupa uhuru kutoka kwa chuki. Watu ambao wamepigana wakawa huru na amani katika mioyo yao na roho. Ushuhuda huu unathibitisha nguvu ya uponyaji ya Mungu, iliyo ndani ya watu kugusa kwa upendo na huruma; hii pia iliiponya mioyo yao, ilibadilisha maisha yao na ikawasamehe. Haijalishi uzoefu wako, asili yako, ngono, unaangaziwa na ugunduzi mkubwa zaidi duniani upendo wa Mungu na fanya mazoezi ya msamaha katika maisha yako mwenyewe.
Hadithi

BAYOMBYA MADULU NDAKI
“Tamaa ya maisha, uporaji na ujambazi, yalipelekea nipigwe risasi, tumbo likafumuka, utumbo wote ukamwagika nje, lakini kwa rehema za Mungu, nikapona. Wenzangu wanne niliohukumiwa pamoja nao, walifia gerezani, mimi peke yangu, nimeokoka na sasa niko huru kuhubiri habari njema. Mungu alinitendea mambo makuu ambayo sitaacha kuyasimulia.”

AMOS HAMIS (Shoga Aliyeokoka)
“Yasiyowezekana kwa binadamu kwa Mungu yanawezekana.” hivi ndivyo ninavyoweza kukiri, ninapoaksi maisha yangu mimi, yaliyosheheni matukio mengi magum ya aibua, yaliyochefua na kusababisha nikataliwe mbali na jamii, ambayo kwa hayo akili za kibinadamu haikuwa vigumu kubadilika, sasa na weza kusema Mungu anaweza kumbadilisha mtu muovu na kumheshimisha tena katika jamii.

WATENDE KIYAGI
Mtoto wa Mitaani
‘Sikuweza kumaliza shule kwa sababu ya ukata ulioikabili familia. Kila nilipopelekwa shuleni, nilitoroka. Nilitorokea visiwani, machimboni na, hata, mijini nikitafuta namna ya kuikwamua familia ili tuondokane na umasikini. Kupitia kutafuta huku, hatimaye, Maisha yangu yakawa ya mitaani. Nilidharaulika, jamii ilinitelekeza na kuonekana kama mtoto asiyefaa. Lakini Mungu, kwa wingi wa rehema, amenufanikisha. Ninamiliki kampuni, nyumba, na magari kadhaa hapa hapa Dar es Salaam.’

MESHAK SALUM HASANI
“Nilionekana kuipenda dini yangu toka utotoni. Na, hata, nilipopelekwa madrasa, nilijisomea kwa bidii na kufikia darasa la sita la Kiarabu.Toka wakati huo, niliendelea na kufuzu kama ustadhi. Kwangu, mimi, dini ilikuwa kila kitu.” Mungu katika ndoto na alinimbia, ‘Hassan, usipoacha uchawi utakufa!’ Sauti ile ilinikosesha amani. Nililazimika kwenda kwenye maombi mlimani, kwa miezi miwili mfululizo,nikimlilia Mungu. Baada ya muda,Mungu alinitahadharisha, ‘Ukitafuta kanisa, litakusaidia.’

JONAS SIMON
Moyoni mwangu, nilijua kuwa ugonjwa niliokuwa nao ulitokana na makosa niliyoyafanya, nilipochochewa na kiburi cha pesa nilizozipata nikiwa kijana. Kila nilipoomba, niliamini kuwa Mungu alinisamehe na,kama ningekufa nikiwa katika hali ile,bila shaka ningeingia mbinguni!Imani hii ilinipelekea kulia mbele za Mungu nikimsihi ili aipokee roho yangu. Maisha yangu yaliyojawa na mashaka sana.Miaka ilienda mbio na, ingawa niliendelea kudhoofu, sikuwa na wasiwasi, Mungu akaniokoa na kuniponya.

BOAZ DAVID MWASOTA
Maisha ya kutumia mihadarati na uporaji yalinitenga mbali na familia. Jamii yangu ilinichukulia kuwa kama ‘mbwa mwitu,’ aliyeishi katikati ya watu. Niliadahika nikidhani kuwa, kwa kufanya hivyo, ningeondokana na upweke. Kumbe haikuwa hivyo! Nilijiongezea matatizo yaliyochangia kujiangamiza kimaisha. Ashukuriwe Mungu aliyeniona, tokea mbali na kunivuta ili kuniingiza katika pendo lake na kuniondolea aibu, leo nathubutu kusimulia matendo yake makuu.”

JAMES YUSTA
Mimi, tofauti na watoto wengine, sikubahatika kumpata mzazi ambaye angenieleza kwa usahihi kuwa nilizaliwa lini na tarehe ngapi! Hata hivyo, ninamshukuru Mungu kuwa nilifanikiwa kupata sehemu ndogo tu ya historia ya maisha yangu, kama nilivyosimuliwa na mama mmoja aliyejulikana kwa jina la YUSTA, aliyeniokoa kutoka katika kinywa cha mbwa aliyekuwa katika hatua za mwisho akitaka kunitafunatafuna!

COSMAS CHIDUMULE
Maisha ya starehe nyingi, nilipokuwa katika ulimwengu wa muziki duniani hayakunifanya nifikie kwenye utoshelevu wa furaha na amani ya kweli moyoni mwangu. Nilipokutana na Yesu na kubadilishwa mwelekeo nikagundua kuwa, furaha na amani ya kweli inapatikana kwake. Sasa naishi nikiwa na matumaini makubwa ya maisha ya milele.

DK. JOE MZIWANDA (Kiongozi wa Dini)
Mafanikio bila Mungu sawa na kujilisha upepo. Ni kuwa na furaha bila amani ya kweli. Niliishi maisha ambayo, licha ya kuwa yenye furaha, sikupata amani ya moyo. Hii ilinipelekea kuwaza sana siku moja na, hatimaye, niliamua kuchukua maamuzi sahihi. Maamuzi yale ndiyo yaliyoniwezesha kupata amani iliyoambatana na furaha niliyoitafuta kwa muda mrefu.”