BOAZ DAVID MWASOTA

Maisha ya kutumia mihadarati na uporaji yalinitenga mbali na familia. Jamii yangu ilinichukulia kuwa kama ‘mbwa mwitu,’ aliyeishi katikati ya watu. Niliadahika nikidhani kuwa, kwa kufanya hivyo, ningeondokana na upweke. Kumbe haikuwa hivyo! Nilijiongezea matatizo yaliyochangia kujiangamiza kimaisha. Ashukuriwe Mungu aliyeniona, tokea mbali na kunivuta ili kuniingiza katika pendo lake na kuniondolea aibu, leo nathubutu kusimulia matendo yake makuu.”

Endelea Kusoma Sikiliza Tazama

JAMES YUSTA

Mimi, tofauti na watoto wengine, sikubahatika kumpata mzazi ambaye angenieleza kwa usahihi kuwa nilizaliwa lini na tarehe ngapi! Hata hivyo, ninamshukuru Mungu kuwa nilifanikiwa kupata sehemu ndogo tu ya historia ya maisha yangu, kama nilivyosimuliwa na mama mmoja aliyejulikana kwa jina la YUSTA, aliyeniokoa kutoka katika kinywa cha mbwa aliyekuwa katika hatua za mwisho akitaka kunitafunatafuna!

Endelea Kusoma Sikiliza Tazama

USHUHUDA WA MUNA LOVE

“MUNGU anazo njia nyingi anazotumia kuokoa watu wake, kwa ajili ya kusudi lake mwenyewe. Alimtumia mtoto wangu akiwa na umri wa miaka sita, kugeuza mtazamo wangu wa imani, siku chache baadaye Mungu alimtwaa. Machungu ya kumpoteza yanazimwa na kauli zake zilizoungamanishwa na upendo wa Mungu ulionivuta mimi kwenye wokovu. Natatangaza fadhili za Bwana katika maisha yangu yote!

Endelea Kusoma Sikiliza Tazama

AMOS HAMIS (Shoga Aliyeokoka)

“Yasiyowezekana kwa binadamu kwa Mungu yanawezekana.” hivi ndivyo ninavyoweza kukiri, ninapoaksi maisha yangu mimi, yaliyosheheni matukio mengi magum ya aibua, yaliyochefua na kusababisha nikataliwe mbali na jamii, ambayo kwa hayo akili za kibinadamu haikuwa vigumu kubadilika, sasa na weza kusema Mungu anaweza kumbadilisha mtu muovu na kumheshimisha tena katika jamii.

Endelea Kusoma Sikiliza Tazama